Watu 75 wanataraji kusimama kizimbani tarehe 17 mwezi
April ,kujibu tuhuma kuhusiana na tuhuma za vurugu zilizotokea wakati
wa mchezo wa soka katika mji wa Port Said nchini Misri miezi miwili
iliyopita na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 70.
Shirika la habari la taifa hilo MENA limetoa taarifa hiyo na kwamba
askari polisi tisa ni miongoni mwa watakao simama upande wa utetezi
katika kesi hiyo ambayo itasikilizwa mjini Cairo kwa sababu za
kiusalama.
Februari mosi mwaka huu, katika mji wa Port Said ,kulitokea vurugu
baina ya mashabiki wa timu za Al- Masry na Al- Ahly kufuatia timu ya Al-
Masry iliyokuwa ikicheza nyumbani kuwavamia na kuwashambulia kwa mawe
na chupa mashabiki wa timu ya Al – Ahly baada ya timu yao kufungwa
magoli 3-1.
No comments:
Post a Comment