NYUMBA YA MZEE ANTHONY WA KASHAI YAUNGUA MOTO.

watu wakijaribu kuokoa baadhi ya mali

Moto ukiongezeka zaidi.


LIVERPOOL KUMKOSA KUYT MSIMU UJAO.


Dirk Kuyt ameihama klabu ya Liverpool
Mchezaji wa safu ya mbele ya Uhalonza Dirk Kuyt ameihama klabu ya Liverpool na kujiunga na Fenerbahce ya Uturuki kwa mkataba wa miaka mitatu. Mshambuliaji huyo anaihama Liverpool baada ya kipindi cha miaka sita.
Kuyt mwenye umri wa miaka 31 alihamia uwanja wa Anfield mnamo mwaka 2006 na kushiriki mara 250 akifunga jumla ya mabao 71.
Taarifa ya Liverpool iliyotolewa kufuatia hatua hio imesema kua Kila mmoja anamtakia Dirk kila la heri na kumshukuru kwa mchango wake.
Aliposajiliwa, Kuyt alisema wakati huo, Kwangu mimi, Liverpool ni ndoto iliyokamilika. Hapana cha kuilinganisha nayo klabu hii, yenye sifa na historia ya kujivunia, alisema.
Mechi yake ya kwanza kushiriki ilikua dhidi ya West Ham United mwezi Agosti mwaka 2006, alipoingia kuchukua mahala pa Peter Crouch ambapo upande wake uliondoka na ushindi wa 2-1.
Bao lake la kwanza lilipatikana mwezi mmoja baadaye alipofunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle.
Baadaye alipendwa na mashabiki wa Liverpool, kivutio kikiwa mchangon wake katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Everton kwenye uwanja wa Goodison Park mwaka 2007 kisha alipofunga 3- peke yake dhidi ya Manchester United, mahasimu wakuu wa klabu kutoka Anfield.
Kuyt ambaye ameshiriki mara 80 kwa Timu yake ya Taifa ya Uholanzi, pia alifunga dhidi ya AC Milan katika mchuano wa Ligi ya mabingwa mwezi May mwaka 2007.
Msimu uliopita mshambuliaji huyo alipata shida kupata nafasi katika kikosi kikuu, akishiriki mara 22 pekee na kuletwa kama mchezaji wa ziada mara tano katika mechi tisa za mwisho wa msimu.
Kwa wakati huu mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka klabu ya Utrecht yuko pamoja na wenzake wa Timu ya Taifa ya Uholanzi wakijinoa kwa ajili ya michuano ya Ulaya 2012 ambapo Wadachi watachuana na Denmark katika mechi yao ya ufunguzi jumamosi ijayo.

Mario Balotelli apinga ubaguzi wa rangi


Mario Balotelli apinga ubaguzi wa rangi
Mario Balotelli nyota wa soka nchini Italia ambaye pia ni mchezaji mweusi wa Klabu ya Manchester City ya Uingereza amesema ataondoka uwanjani endapo atakejeliwa kutokana na rangi yake wakati wa mchuano wa kombe la Mataifa Ulaya katika nchi za Poland na Ukraine mwezi Juni.
Matamshi yake yanatokea kufuatia makala ya BBC ambayo yaliangazia ghasia katika viwanja vya soka kutokana na ubaguzi wa rangi katika nchi hizo mbili.
Makala hayo yalionyesha mashabiki wakizungu wakiwakejeli wachezaji weusi na kuwashambulia mashabiki wenye asilia tofauti na kizungu.
Wanasiasa na maafisa wa soka kutoka nchi hizo wamesema tatizo hilo limetiwa chumvi.
Kukejeliwa kwa ubaguzi wa rangi dhidi ya Balotelli nchini Italia mwaka 2009 kulifanya shirika la soka Ulaya UEFA kuweka sheria ya kuwalazimisha marefa kusimamisha mechi ikiwa kejeli za ubaguzi wa rangi zitaendelea.

SAJUKI, MWACHENI MUNGU AITWE MUNGU

SAJUKI, MWACHENI MUNGU AITWE MUNGU HEBU mwacheni Mungu aitwe Mungu! Hatimaye habari njema kutoka katika Hospitali ya Saifee iliyopo jijini Mumbai, India anakotibiwa staa wa filamu za Kibongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ zinatia faraja kwa Watanzania, Ijumaa Wikienda linakupa stori ‘exclusive’ kutoka nchini humo.

Habari hizo njema zinaeleza kuwa Sajuki aliyeambatana na mkewe, Wastara Juma na kaka yake, hatimaye ameweza kunyanyuka kitandani na kuongea tofauti na siku aliyoondoka Bongo na mwanzoni alipofikishwa hospitalini hapo.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mwishoni mwa wiki iliyopita kwa njia ya simu, Wastara alisema Sajuki alikuwa amepata nafuu na hali siyo mbaya kwani alikuwa na uwezo wa kuzungumza hivyo akampa simu ili azungumzie afya yake yeye mwenyewe jinsi anavyojisikia.


Sajuki alipopewa simu alianza kwa kuwashukuru wale wote wanaomuombea dua na kujitolea kwa hali na mali ili kuokoa uhai wake.
“Namshukuru sana Mungu naendelea vizuri. Nilichukuliwa vipimo na nikabainika kuwa na uvimbe mwingi sehemu mbalimbali tumboni.
“Madaktari walibaini kuwepo kwa uchafu kwenye mapafu. Mwanzoni waligundua nina tatizo la kupumua na kukaukiwa damu.
“Wamelishughulikia hilo kwanza na hapa nilipo nimezungukwa na madawa, kwa kweli najisikia nafuu,” alisema Sajuki kwa sauti ya kukwaruza.


Sajuki alisema alipokelewa vizuri lakini kabla ya kuanza matibabu ya uvimbe tumboni, madaktari walilazimika kumtibu kwanza tatizo la damu na pumzi hivyo matibabu ya kilichompeleka hospitalini hapo (uvimbe) yakawekwa pembeni.

Kwa upande wake, Wastara alisema kuwa Sajuki alipaswa kupatiwa matibabu kwa wiki mbili ndipo warejee nyumbani lakini kwa hali halisi inaonekana watakaa zaidi kwani tayari wiki mbili zimekatika.

Wastara alisema kuwa baada ya kumalizika kwa tatizo la pumzi na kupungukiwa damu, madaktari wameanza vipimo vya tatizo la uvimbe na kusisitiza kuwa uzi ni uleule wa kumwombea mumewe ili arejee katika siha njema.

Sajuki alianza kusumbuliwa na uvimbe mwaka jana ulioanzia mkononi na baadaye ndani ya mwili kwenye ini na sasa madaktari wanasema siyo kwenye ini tu bali na sehemu nyingine tofauti za tumboni.

Kama alivyosema Wastara, tuzidi kumuombea dua Sajuki ili arejee katika ulingo wa filamu aendelee kutuelimisha na kutuburudisha tunapokuwa majumbani mwetu.

ZITTO AAMSHA BALAA

Zitto aamsha balaa,Atoboa yalipokwa kinyemela kwenye Muungano Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), Zitto kabwe, amefufua hoja ya nafasi ya mafuta na gesi kuwa mambo ya Muungano na amesema bila kumung’unya maneno kuwa suala hilo kuendelea kubakia kama lilivyo, ni kuendeleza makosa.
Zitto ambaye pamoja na wabunge wenzake walikuwa Uholanzi kwa ziara ya kujifunza jinsi nchi hiyo inavyoendesha sekta ya mafuta ya petroli na gesi na kurejea hivi karibuni, ameandika makala ndefu kuhusu mafuta na gesi kuwa mambo ya muungano na kuipa kichwa cha habari “Mafuta kuwa suala la Muungano tulikosea.”
Kwa kauli yake, Zitto amesema kuwa ni dharau kwa Wazanzibari kuwaambia kuwa mafuta na gesi ni masuala ya Muungano wakati hakuna uwazi jinsi suala hilo lilivyoingizwa katika orodha hiyo, licha ya serikali kuwa na majibu mepesi.
“Katika moja ya vikao vya Bunge katika Bunge la Tisa, aliyekuwa Naibu wa Waziri wa Nishati na Madini Ndugu Adam Malima alileta kumbukumbu za mjadala Bungeni (Hansard) za mjadala wa suala la mafuta na gesi ili kuthibitisha kwamba jambo hili halikuuingizwa kwenye Katiba kinyemela,” alisema Zitto katika makala hiyo aliyoiweka kwenye ovuti yake jina la zittokabwe.wordpress.com.
Amesema wakati Muungano unaanzishwa mwaka 1964 mafuta na gesi hayakuwa masuala ya Muungano na kwamba baada ya kueangalia katika Hati ya Muungano ambayo ilikuwa ni sehemu ya Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1965, suala hilo halikuwamo katika orodha ya mambo 11 ya Muungano.
“Nyaraka nilizoziona zinaonyesha kwamba suala la mafuta na gesi asilia liliongezwa katika orodha ya Mambo ya Muungano mwaka 1968.
Kuna watu wanahoji kihalali kabisa kwamba nyongeza ya jambo hili ilifanywa bila kufuata taratibu na hivyo kufanywa kinyemela na kuna wengine wanasema jambo hili lilifuata taratibu zote za kisheria ikiwemo kupigiwa kura na Bunge la Muungano na kuungwa mkono na theluthi mbili ya wabunge kutoka pande zote za Muungano,” anasema.
Hata hivyo, Zitto anafafanua kuwa wakati umefika kwa watafiti wa masuala ya Muungano kupekua nyaraka hizo na kusema ukweli  namna suala la mafuta na gesi lilivyoingizwa katika orodha ya mambo ya Muungano.
Alisisitiza kuwa  jambo hilo sasa ni  la Muungano kwa mujibu wa Katiba na ni dhahiri kuwa Watanzania wa Wazanzibari hawafurahishwi nalo na hivyo kuazimia kupitia Azimio la Baraza la Wawakilishi kwamba jambo hilo liondolewe kwenye orodha ya masuala ya Muungano, ameshauri kuwa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inapaswa kutoa uamuzi wa mwisho utakaomaliza mjadala huu.
Zitto katika makala hito amesema kuwa licha ya Bunge la Muungano kuamua kuongeza suala la mafuta na gesi asilia katika masuala ya Muungano, mwaka mmoja baada ya uamuzi huo liliundwa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa amri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano (establishment order).
“Shirika hili halikuanzishwa kwa Sheria ya Bunge au kwa Sheria ya Makampuni kama yalivyo Mashirika mengi ya Umma hapa nchini bali kwa amri ya Rais … Katika amri hii ya Rais, Shirika la TPDC halikupewa ‘mandate’ (mamlaka ) ya kimuungano.
Shirika hili mipaka yake ilianishwa kuwa ni Tanzania Bara peke yake. Hivyo suala la Muungano likawekewa Shirika la Tanganyika kulisimamia!” Zitto anabainisha katika makala ndefu kuwahi kutolewa na Mbunge huyo tangu suala la mafuta na gesi litikise nchi kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Mbunge huyo ambaye mwaka 2007 alipata kuamsha moto mkubwa juu ya kampuni za madini ya Barrick kushirikiana na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kusaini mkataba wa mgodi wa Buzwagi ughaibuni, alisema TPDC imekuwa ikifanya kazi ya kusimamia sekta ya mafuta na gesi ikiwemo kutoa vibali vya kutafuta mafuta, kuingia mikataba na makampuni ya kimataifa na kuisimamia mikataba hiyo.
Alitaja miongoni mwa mikataba hiyo ni kwenye maeneo ambayo kama isingekuwa Muungano yangekuwa ni maeneo ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kwamba mbaya zaidi mikataba yote ya utafutaji na uchimbaji mafuta inafanywa inaingiwa na Waziri wa Nishati na Madini Wizara ambayo siyo ya Muungano.
“Hakuna hata eneo moja ambalo taratibu zimewekwa kwamba pale ambapo eneo hilo ni eneo lilikuwa chini ya himaya ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar basi mikataba isainiwe na Mawaziri wawili wa sekta hiyo kutoka kila upande wa Muungano,” anabainisha katika makala hiyo.
Zitto ametoboa siri katika kakala hiyo akisema kuwa miaka ya mwanzo ya 2000 TPDC iliingia mikataba ya vitalu kadhaa vya mafuta miongoni mwake ni nambari  9, 10, 11 na 12 mashariki ya visiwa vya Pemba na Unguja, pia Shirika hilo na Wizara ya Nishati waliingia mkataba mwingine katika kitalu kilichopo kati ya Pemba na Tanga (mahala ambapo kumekuwa na dalili za wazi za kuwapo mafuta kutokana na kuonekana kwa ‘Oil sips’ mara kwa mara.
“Vitalu 9, 10, 11 na 12 vilipewa kampuni ya Shell ya Uholanzi na kitalu cha kati ya Tanga na Pemba walipewa Kampuni ya Antrim ya Canada ambayo baadaye waliuza sehemu ya Kampuni yao kwa Kampuni ya RAK Gas kutoka Ras Al Khaimah huko United Arab Emirates.
Kwa kuwa Vitalu hivi vipo katika eneo la iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kabla ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikataa shughuli zozote kufanyika mpaka suala la Mafuta na Gesi kuondolewa katika orodha ya Mambo ya Muungano lipatiwe ufumbuzi,” ametoboa.
Alisema uamuzi wa Serikali ya Zanzibar ungechukuliwa na Serikali yeyote ile yenye mapenzi ya dhati na watu wake.
“Uamuzi huu ulileta mjadala mpana sana katika masuala ya Muungano na ambao hawana taarifa waliubeza sana.
Hata hivyo suala hili likafanywa ajenda katika vikao vya masuala ya Muungano vinavyoitwa Vikao vya Kero za Muungano. Miaka kumi suala hili linajadiliwa na Maamuzi hayafanyiki! Hivi sasa kila suala lenye kuangukia kwenye Katiba husukumwa huko na hivyo kutoa ahueni kwa wanaogopa kufanya maamuzi,” amesema.
Zitto ameshauri kuwa kwa hali ilivyo sasa mambo makuu mawili yafanyike kuhusu sekta ya mafuta; “ushauri wangu ni kwamba; kwa maana ya kuandikwa kwenye Katiba mpya ni kwamba suala la mafuta na gesi asilia liendelee kuwa suala la Muungano kwenye eneo la usimamizi wa Tasnia na leseni za utafutaji (Upstream Regulatory mechanism).
Hili ni eneo linalohitaji usimamizi wa dhati kabisa na kwa pamoja pande mbili za Muungano zinaweza kufanya vizuri zaidi.”
Pili, ananshuri kuwa: “Eneo la Uchimbaji na hasa kugawana mapato ya mafuta na Gesi (Profit Oil) lisimamiwe na kila upande wa Muungano kivyake.
Biashara ya Mafuta isiwe jambo la Muungano na hivyo kila Upande wa Muungano uwe na shirika lake la mafuta na gesi ambalo litashiriki kama mbia wa mashirika ya kimataifa katika uchimbaji, usafirishaji na uuzaji wa mafuta na gesi asilia.
Mapato yanayotokana na Mafuta (Profit Oil) na kodi nyingine zote isipokuwa mrahaba (royalty) yawe ni masuala yanayoshughulikiwa na Serikali ya kila upande wa Muungano kwa mujibu wa Sheria ambayo Serikali hizo zimejiwekea.”
Zitto amesema kuwa kwa sasa Tanzania inakadiriwa kuwa gesi iliyogunduliwa ikiwa na ujazo wa futi trilioni 20; huku Msumbuji ikiwa na futi za ujazo trilioni 107, Angola chini ya futi za ujazo trilioni 100, Algeria futi za ujazo trilioni 100 na Nigeria ikiwa inaongoza kwa kuwa na futi za ujazo trilioni 189; ikiongoza barani Afrika. Kwa utajiri huo, anasema haitawezekana kuacha suala mafuta na gesi bila ufumbuzi katika mvutano wa Zanzibar na Tanzania bara.

MZEE BWIKIZO AFARIKI DUNIA

Habari tulizo pata muda mfupi za kuhusu kifo cha mzee wa kashai,SULEIMANI BWIKIZO ni zakusikitisha sana sana.Maiti itasafirishwa kupelekwa kijijini kwao Kesho na mazishi yatafanyika Majira ya mchana.HABARI ZIKUFIKIE WEWE UNAESOMA HABARI HII PIA WAAMBIE NA WENZAKO.MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEM MAHALI PEMA PEPONI.Aaaamin

MAWAZIRI WA JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA WAAPA ASUBUHI HII IKULU


 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika viwanja vya Ikulu asubuhi hii ili kuanza kazi ya kuapisha mawaziri wapya aliowateua hivi karibuni Fullshangweblog ikiwa katika viwanja vya Ikulu inashuhudia kuapishwa huku kwa mawaziri na kukuletea moja kwa moja kutoka viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam.
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza na Katibu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue kabla ya kuanza kwa kuapiswa mawaziri hao.
 Dk. Harrison Mwakyembe akila kiapo kuwa waziri wa Uchukuzi mbele ya Rais Jakaya Kikwete kwenye viwanja vya Iku asubuhi hii.
 Shamsi Vuai Nahodha akila kiapo kuwa waziri wa Ulinzi mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
Dk Husein Mwinyi akila kiapo kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
 Profesa Jumanne Maghembe akisaini kiapo mara baada ya kuapa kuwa waziri wa  maji na umwagiliaji
 Hawa Ghasia akila kiapo
 Mh. Mathias Chikawe waziri wa Sheria na Katiba.
Mh. George Mkuchika akipongezwa na Rasi mara Baada ya kula kiapo.